DOLA FEKI ZATUMIKA MIAKA 20 BILA KUJULIKANA

WAKATI Marekani
ikijinasibu kama Taifa lenye intelijensia kali na bora kuliko wote duniani,
habari mbaya kwao ni kwamba zimegundulika fedha bandia, dola za nchi hiyo,
ambazo zimeingizwa katika mzunguko na kufanya kazi kwa zaidi ya miaka 20 bila
kugundulika.
Noti hiyo ya dola
bandia haikuwa na makosa yoyote na hata maafisa wa kitengo cha ujasusi
hawakuweza kubaini iwapo ilikuwa dola bandia ama nakala halisi mbele yao.
Ni baada ya kipindi
kirefu cha uchunguzi ndipo waliweza kuthibitisha kwamba zilikuwa hela bandia.
Lakini noti hizo za
dola mia moja zilikuwa hazina dosari yoyote hadi zikapewa jina ''The Super fake
Dollars''.
Zilikuwa na rangi
kama ile ya noti halisi za dola za Marekani.
Pia zilichapishwa
katika karatasi iliyokuwa sawa na ile ya pesa halisi ikiwa na robo tatu ya
pamba na robo ya kitani (linen).
Picha ya noti hizo
ilikuwa bora zaidi ya zile zilizochapishwa na shirika la kuchapisha fedha
Marekani.
Mashine ya kuhesabu
noti katika benki pia zilishindwa kubaini uhalisia wake. Zilikuwa na tofauti
kidogo sana, wakati Gazeti la The New York Times liliporipoti kwamba fedha hizo
hazikuwa halisi, Marekani lishangazwa kwamba fedha bandia ziliweza kupita benki
zake bila kujulikana , kwa sababu hakuna aliyeweza kubaini tofauti.
Fedha hizo za Super
Dollars zilisambaa kote duniani kati ya miaka 1990 na 2000.
Wakati wa miaka hii,
Marekani iliamua kubadilisha noti ya dola 100 mara mbili lakini watengenezaji
wa fedha hizo bandia walifanikiwa kubadilisha fedha hizo na kufanana kama zile
zinazochapishwa na serikali.
Zilipatikana nchini
Denmark, Ufaransa, Austria, Ujerumani, Latvia, Urusi, Czech Republic na Ireland.
Wahalifu nchini
Urusi walizitumia bila aibu.
Kwa miaka kadhaa
zilikuwa mwiba kwa shirika la ujasusi la Marekani FBI.
Hawakujua ni nani
aliyekuwa akizichapisha, Ilichukua operesheni kali ya miaka minane ili kuanza
kuwakamata wahusika.
Walifanikiwa
kuwakamata washukiwa wa kwanza mjini California na New Jersey, baada ya
wachunguzi kupata makasha ya fedha hizo kutoka katika meli kutoka kusini
mashariki mwa bara Asia.
Wale waliokamatwa
walikuwa na uhusiano na wahalifu wa kimataifa, lakini maafisa wa shirika la FBI
walikuwa wakishuku kwamba mtandao huo ulikuwa mkubwa zaidi.
Fedha hizo
hazikutengenezwa na wahalifu wa kawaida ama mtandao wa wahalifu, lakini
zilitengenezwa na serikali ya Korea Kaskazini... Serikali ya Marekani ilisema.
Mara kwa mara fedha
hizo zilipatikana katika mikono ya wanadiplomasia wa Korea Kaskazini, pengine
kuongeza mapato ya taifa hilo ambalo lilikuwa likikumbwa na matatizo ya njaa na
kuanguka kwa mshirika wake mkuu Muungano wa Usovieti.
Hata hivyo Korea
Kaskazini inakana kuhusika katika kuchapisha fedha hizo.
''Korea Kaskazini
imekana kuhusika katika usambazaji na uchapishaji wa sarafu bandia , lakini ushahidi
unaonesha wazi kwamba ni wao'', alisema Daniel Glazer, Naibu Waziri wa Masuala
ya Uhalifu wa kifedha akizungumza na New York Times.
''Hakuna maswali yoyote
juu ya kuhusishwa kwa Korea Kaskazini'', alisema.
Mamlaka nyingine
zilitaja kughushi huko kama shambulizi baya la mfumo wa fedha wa Marekani.
Hata hivyo ,
kipaumbele cha FBI kilikuwa kusitisha usambazaji wa fedha hizo katika taifa la
Marekani.

Post a Comment