RPC DAR AANZA KAZI KWA KISHINDO

  

Wambura replaces Mambosasa as Dar es Salaam Regional Police Commander - The  Citizen

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum y Dar es Salaam, ambaye aliteuliwa hivi karibuni, ameanza kazi kwa kishindo cha aina yake baada ya kutoa taarifa kuhusu kukamatwa kwa majambazi na bidhaa kadhaa zilizoibiwa.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linaendelea na Operesheni Maalum ya kupambana na vitendo vya kihalifu Katika maeneo yote ya Jiji la Dar es Salaam katika dhima nzima ya Usalama wa Raia na Mali zao na limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 20 na vielelezo mbalimbali kama ifuatavyo:-

 

1. Majambazi watano wapora silaha wakamatwa

Mnamo tarehe 18/03/2021 majira ya saa 8.00 usiku majambazi wapatao watano walivamia katika nyumba ya Mkurugenzi wa Benki ya Azania iliyopo Mbweni Mpiji na kuwashambulia walinzi wa kampuni ya SUMA JKT na kuwapora silaha aina ya Short Gun Pump Action ikiwa na risasi tano.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM lilifanya ufuatiliaji na kufanikiwa kukamata silaha hiyo tarehe 20/05/2021 na watuhumiwa watano waliohusika katika tukio hilo.

 

2. Watano washikiliwa kwa mauaji

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya DSM linawashikilia watu watano kwa tuhuma za mauaji.

 

Watuhumiwa hao ni:-

 

1. Issa Karim@ Mdaka Bomu, Miaka 33, Mkazi wa Mbezi

2. Mohamed Juma@Mabangi, Miaka 31, Mkazi wa Mbezi Mwisho

3. Selemani Seif@Dullah Kishandu, Miaka 34, Mkazi wa Mbezi Mwisho.

4. Samsoni Joseph mjeuri, Miaka 32, Mkazi wa Mbezi

5. Ezekiel Kennedy@Simba MC,Mkazi wa Mbezi

 

Ambapo, mnamo tarehe 08/05/2021 majira ya 8:05 usiku huko Mikocheni A watuhumiwa hawa walivamia katika bar iitwayo Imbizo Bar na kumshambulia kwa mapanga na marungu mlinzi aliyefahamika kwa jina Regan Sylivester na kusababisha kufariki dunia papo hapo.

Aidha watuhumiwa wanahusika na tukio la unyan’ganyi wa kutumia silaha huko Mabwepande ambapo mnamo tarehe 07/05/2021 majira ya 09:00 usiku walivamia katika kituo cha kuuzia Mafuta (Petrol station) cha MEXONS na kuwashambulia walinzi, wahudumu na wateja na kupora kiasi cha Tsh 2, 440,000/= na kisha kupora silaha aina ya Short Gun ya walinzi hao.

3. Pikipiki, magari manne yaliyoibwa yakamatwa

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam limefanikiwa kukamata magari manne na watuhumiwa wanne.

Watuhumiwa hao ni :-

1. Babuelly Simon Chao, Miaka 43,Mkazi wa Moshi

2. Sebastiani Shembaru, Miaka 36, Mkazi wa Kigamboni

3. Hussen Misanya, Miaka 33, Mkazi Mabibo Relini.

4. Said Rajabu, Miaka 16, Mkazi wa Mabibo

Watuhumiwa hawa wamekuwa wakiiba magari maeneo ya Kinondoni na Ilala na walikamatwa na magari yafuatayo:-

 

1. T 817 ATQ Toyota Nadia

2. T 134 BPJ Toyota IST

3. T 952 CKB Toyota Mark II Grand

4. T 590 DTK Toyota IST

Aidha, Jeshi la Polisi Kanda Maalum DSM limefanikiwa kukamata Pikipiki namba MC 136 CSA Boxer nyeusi iliyokwa imeibiwa tarehe 15/05/2021 huko maeneo ya Kibamba shule na kupelekwa Gairo Mkoani Morogoro.

Jeshi la Polisi Kanda lilifanya ufuatiliaji na kufanikiwa kuikamata pikipiki hiyo na kuirudisha Jijini DSM.

4. Watano washikiliwa kwa kuvunja na kuiba usiku

Mnamo tarehe 23/05/2021 majira ya saa 08:30 usiku huko Mtaa wa Mikocheni A walivunja nyumba ya Daud Ramadhani na kuiba vitu mbalimbali.

Watuhumiwa wamekamatwa wakiwa na baadhi ya mali walizoiba ikiwa ni pamoja na TV moja aina ya LG NCH 55 Flat screen,Simu mbili aina ya iphon, Laptop mbili aina ya Dell na Mouse nne za kompyuta.

Watuhumiwa hao ni:-

1. Abeid Said@Gebe, Miaka 41, Mkazi wa Kinondoni

2.Laurent Mwazembe, Miaka 44, Mkazi wa Malamba Mawili.

3.Ramdhani Mohamed, Miaka 31, Mkazi wa Mbezi

4.Julias Mapunda,Miaka 34, Mkazi wa Mbezi Njeteni

5.Emmanuel Zongo, miaka 30, mkazi wa Kigamboni

 

5. Sita washikiliuwa kwa uvunjaji

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linawashikilia

watu sita (6) kwa tuhuma za uvunjaji maduka usiku na kuiba.

Watuhumiwa hao ni :-

1. Kaburu Mohamed kaburu,(30),Mkazi wa Buza Kanisani.

2. Iddi Ally Kiduku, Miaka 30, Mkazi wa Tandika.

3. Said Ramadhani @Timu, Miaka 33, Mkazi wa Kitunda.

4. Lucas Danford@Udongo wa Maka, Miaka 31, Mkazi wa Buguruni

5. Shaban Bakari@Majani, Miaka 33, Mkazi wa Tandika kaburi moja.

6. Khamis Bahati Chief, Miaka 38, Mkazi wa Buza kwa mama kibonge.

Watuhumiwa hawa wamekuwa wakijihusisha na vitendo vya uvunjaji maduka nyakati za usiku katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam hususani katika mitaa ya Kariakoo na Ukonga Banana.

ONYO, Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam linatoa onyo kali kwa wahalifu wanaojihusisha na vitendo vya kihalifu waache mara moja kwani Jeshi lipo imara na limejipanga vizuri kuhakikisha hali ya Jiji inaendelea kuwa shwari.

 

Camillius M.Wambura - SACP

KAMANDA WA POLISI,

KANDA MAALUM,

DAR ES SALAAM.

25/05/2021

No comments