MBOWE AONGOZA KIKAO CHADEMA ARUSHA

 

Chadema chairman Freeman Mbowe to be a free man today - The Citizen

MWENYEKITI  wa Taifa wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe leo ameongoza kikao cha Kamati ya Utendaji Kanda ya Kaskazini kilichofanyika jijini Arusha.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumanne tarehe 25 Mei 2021 na Chadema, kupitia ukurasa wake wa Twitter, chama hicho kina mpango wa kuzindua kile kilichoitwa Operesheni Haki hapo Alhamisi.

Taarifa ya Chadema imesema kuwa, lengo la operesheni hiyo ni kudai katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, pamoja na uimarishwaji misingi ya haki nchini.

“Leo Mei 25, 2021, Mwenyekiti wa chama Taifa, Freeman Mbowe, ameendesha Kikao cha Kamati Tendaji ya Kanda ya Kaskazini, jijini Arusha,” imesema taarifa ya Chadema.

 

No comments