RC MAKALA ATAKA MAJAMBAZI DAR WAPEWE SHOW KALI

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makala amewataka Polisi kuhakikisha wanafanya kila wawezalo ili waweze kudhibiti wimbi jipya la ujambazi lililoibuka kutoka kusikojulikana.
Akizungumza jijini
hapo jana, Makala ambaye alipata kuwa mkuu wa mkoa wa Mbeya, moja ya mikoa
korofi kwa uhalifu, alisema majambazi hao wamekuja na moto, hivyo dawa ya moto
ni moto.
"Nataka Polisi
wawape show kali hawa majambazi, wanyang'anywe silaha kabla
hawajazitumia," alisema.
Kwa zaidi ya miaka
mitano, uhalifu ulionekana kutoweka hasa jijini Dar es Salaam na sehemu kubwa
ya nchi, lakini mara tu baada ya kifo cha Rais John Joseph Magufuli, hali
inaonekana kubadilika ghafla, kitendo kilichomfanya Rais Samia Suluhu Hassan
kukisema hadharani, akimtaka IGP Simon Sirro kuchukua hatua.

Post a Comment