TISHETI YA KIKWETE YAWA GUMZO

KWA kawaida Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete ni mtu mwenye tabasamu muda mwingi usoni kwake. Ni nadra kumuona akiwa amefura kwa hasira.
Maandishi yaliyoandikwa katika
tisheti anayoonekana ameivaa, ni kama yamewachanganya watu, kwani hayaendani na
uhalisia wake. Imeandikwa hivi: KASI ISAMBAZAYO TABASAMU.
Sawa, yeye ni shabiki wa Yanga,
lakini mabingwa hao wa kihistoria wana kasi gani inayosambaza tabasamu kwa
mashabiki wake?
Bila shaka hiki ni kijembe cha
kisiasa kwa wanasiasa.
Maneno haya yana maana kubwa sana yanapokaa mgongoni mwake
tofauti na yangekaa mgongoni mwa mwananchi wa kawaida.

Post a Comment