RAIS AKUTANA NA TAJIRI NAMBA MOJA AFRIKA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassani, leo amekutana na kufanya mazungumzo na tajiri namba moja barani Afrika, Alhaji Aliko Dangote, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Alhaji Dangote ambaye ni Mnigeria na mfanyabiashara mkubwa
duniani, ni mwekezaji nchini Tanzania akiwa amewekeza katika Kiwanda Cha Saruji
cha Dangote kilichoko mkoani Mtwara.
Alhaji Dangote amemshukuru Rais Samia kwa kuboresha mazingira
ya Uwekezaji nchini na ameahidi kuwa ataendelea kuwekeza Tanzania kwenye maeneo
tofauti ikiwamo ujenzi wa Kiwanda cha Mbolea,
Kwa upande wake, Rais Samia aliahidi kuwa Serikali yake
itaendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini kwa faida ya pande zote na
aliwaagiza mawaziri husika kushughulikia changamoto zinazoikabili Kampuni ya
Dangote.

Post a Comment