FRED VUNJA BEI APENYA UVCCM


Vunja bei.png

 YULE mfanyabiashara wa nguo aliyeshinda dili kubwa la zaidi ya bilioni mbili ili kuuza na kusambaza jezi za Simba, amepenya tena, safari hii ndani ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM).

Mfanyabishara huyo mwenyeji wa Makete mkoani Iringa, Fredy Ngajiro Maarufu Kama Fred Vunjabei ameteuliwa Kuwa Mwenyekiti Wa Kamati Ya Fedha Ya Uvccm.

Fred Ngajiro amepitishwa na Baraza kuu la UVCCM kuwa Mwenyekiti mpya wa kamati ya Uchumi, Uwezeshaji na Fedha kupitia kikao cha Baraza Kuu ambacho kimemalizika jana Makao Makuu ya CCM Dodoma.

Kamati ya utekelezaji chini ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Kheri James ilikuja na pendekezo la jina la mwenyekiti huyo wa kamati ambapo baadae alithibitishwa na wajumbe kwa kura nyingi za ndio huku katibu wake akifahamika kwa jina la Rose Manumba, Baraza lilichagua wajumbe wengine wanne wa kamati kutoka bara na visiwani.

 

No comments