OLE SABAYA AKAMATWA, ANAHOJIWA


Haki Ngowi on Twitter: "MKUU wa Wilaya ya Hai, mkoani Kilimanjaro, Lengai Ole  Sabaya, akilia kwa uchungu wakati wa shughuli za kuuaga mwili wa Hayati Dk.  John Pombe Magufuli, Uwanja wa Jamhuri

 ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya ambaye alisimamishwa na Rais Samia Suluhu Hassan ili kupisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili, imeripotiwa kuwa kiongozi huyo amekamatwa na vyombo vya dola na sasa anahojiwa.

Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika, Sabaya amehojiwa na vyombo vyote vya dola na wakati wowote atapandishwa kizimbani.

Miongoni mwa tuhuma dhidi yake ni pamoja na kuwabambikia watu kesi, kuhusika kupora fedha kwa kutumia nafasi yake, kunyanyasa raia na kufanya kazi zisizomuhusu, kama kudai kodi.

 

No comments