NANI KAMUUDHI PROFESA JAY?
UTANIAMBIA NINI ndiyo ngoma mpya ya mkongwe wa Hip Hop Tanzania, Joseph Haule maarufu kama Profesa Jay iliyotoka wiki chache zilizopita na sasa inapata mileage ya kutosha katika redio nyingi hapa nchini.
Ukisikiliza
mashairi ya mkongwe huyo, unaona kabisa kaimba kwa hisia, kitu kama kimemuuma
kwa muda mrefu na sasa kaamua aseme.
Tena aliyemkera
anaonekana kuwa bwa mdogo tu, maana ndani ya wimbo huo anasema 'Utaniambia
nini, nimeanza kuimba kabla yako. Nimeshakula sana bata kabla yako na kama ni
ng'ambo, nishatimba kitambo kabla yako.
'Hata mjengoni
nilikuwa na baba yako au mama yako..... yaani kifupi, Mzee wa Mitulinga
kachafukwa.
Nani kamkera, Ojuku
Blog inamtafuta amwage ukweli...

Post a Comment