MWANAMKE ALIWAGOMBANISHA CHEGE NA NATURE

IMEVUJA. Aliyewahi kuwa kiongozi wa kundi la T.M.K Wanaume Family, Said Fella maarufu kama Mkubwa, ametoboa siri kuwa ugomvi kati ya nyota wa kundi hilo, Juma Kassim 'Nature' na Said Chigunda 'Chege' ulisababishwa na mwanamke.
Fella ambaye hivi
sasa ni mmoja wa mameneja wa Diamond Platnum katika kampuni ya WCB, alisema
awali mwanamke huyo alikuwa ni mali ya 'mtoto wa Mama Said', lakini baadaye
akageuka na kumtaka Nature, ambaye enzi hizo alikuwa msanii mkubwa kuliko
Chege.
Mwanzoni mwa miaka
ya 2010, Nature alijiondoa katika kundi la TMK Wanaume Family na kuanzisha TMK
Wanaume Halisi akiwa pamoja na swahiba wake wa tangu utotoni, Haruna Kahena
'Inspekta'.

Post a Comment