MPOKI ADOKEZA 'WALIVYOPENYA' UGOMVI WA MANJI NA MENGI

MCHEKESHAJI mahiri hapa nchini, Mpoki amedokeza jinsi ugomvi kati ya wafanyabiashara maarufu nchini, marehemu Reginald Abraham Mengi na Yussuf Manji ulivyowapelekea wao 'kutoboa'.
Mpoki pamoja na wenzake Masanja Mkandamizaji,
Joti, Mac Reagan chini ya Seki, walikuwa na kundi lao la Comedy, wakirusha
vichekesho vyao katika televisheni ya ITV.
Lakini katika kile kilichoonekana kuwa ni
masilahi, kundi hilo liliingia katika mzozo na mzee Mengi na hivyo kuwafanya
wajiondoe.
“Matajiri wakigombana, maskini anapita katikati...” amesema
Mpoki na kueleza kwamba Manji aliwapa mkataba mnono, akawasafirisha kwenda
Uingereza.
Akizungumza katika kipindi cha Joto la Asubuhi kinachorushwa
na kituo cha redio cha EFM, Mpoki anasema ugomvi wao na mzee Mengi ulikuwa
mkubwa ambao licha ya kushindikana mahakamani, ulimalizwa na aliyekuwa Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda.
Katika hatua nyingine, mchekeshaji huyo ambaye
pia ni mtangazaji wa kituo hicho, alisema hapendi kuyaanika maisha yake
binafsi, yeye na familia yake.

Post a Comment