MORRISON ATHIBITISHA THAMANI YAKE NDANI YA SIMBA

IKICHEZA mechi yake ya 26 leo katika Uwanja wa Majaliwa kule Luhangwa, Lindi, timu ya Simba ilikuwa nyuma kwa bao moja hadi wakati wa mapumziko.
Wengi wakiamini
kwamba huu utakuwa mchezo mgumu kwa mabingwa hao watetezi, na hasa baada ya
Namungo kuanza kujiangusha ovyo wakiamini wanashinda, kocha Didier Gomes Da
Rosa alifanya mabadiliko kwa kuwatoa Larry Bwalya, Meddie Kagere na Konde Boy,
wakitoa nafasi kwa Hassan Dilunga, John Bocco na Benard Morrison.
Wakiwa nyuma kwa
bao hilo moja, Simba walisawazisha kupitia kwa Chris Mugalu, aliyeungankisha
krosi kutoka kwa beki Shomari Kapombe ambaye alipenyezewa penetration pass na
HD.
Simba wakapata bao
la pili ambalo lilifungwa na John Bocco kufuatiwa pasi safi kutoka kwa Mugalu,
ambaye naye alipewa pasi ile na HD.
Lakini burudani ya
wanamsimbazi ilihitimishwa na Bernad Morisson ambaye alithibitisha thamani yake
ndani ya kikosi hicho.
Hassan Dilunga
alilazimika kulala ili kuutoa mpira miguuni mwa mchezaji wa Namungo katikati ya
uwanja, mpira huo ukamfikia Morisson, ambaye aliusogeza kidogo tu kutoka umbali
wa zaidi ya mita 40, akamtazama kipa wa Namungo kisha akaupiga mpira mrefu
uliomaliza mechi ya leo kwa Simba kushinda kwa bao 3-1.

Post a Comment