MO: SITANUNUA FERARI TENA NA ROLLS ROYCE, NITAWEKEZA ZAIDI SIMBA

 Mapinduzi Cup: Simba SC chairman Dewji resigns after losing the final |  Goal.com

MWEKEZAJI wa Klabu ya Simba ya jijini Dar es Salaam, Mohamed Ghulam Dewji maarufu kama Mo, amesema amesitisha mpango wake wa kujizawadia gari la kifahari aina ya Ferari aliokua amepanga na badala yake atawekeza zaidi kwa timu yake ili kuwapa furaha watu wengi zaidi.

Kupitia katika akaunti yake ya Instagram, tajiri huyo namba moja kijana barani Afrika amesema furaha ya mashabiki wa Simba kwake ni muhimu zaidi kuliko furaha yake binafsi.

Maelezo hayo, bila shaka, yanakuja baada ya jana kuishuhudia timu yake ikipokea kipigo cha mbwa mwizi cha mabao 4-0 kutoka kwa Kaizer Chiefs katika mchezo wa kwanza wa robo fainali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kule Johannesburg Afrika Kusini licha ya timu yake kutandaza soka safi.

 

No comments