MO AKANDIA NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA AFRIKA

KATIKA kile kinachotafsiriwa kama hasira, mwekezaji ndani ya Simba, Mohamed Ghulam Dewji maarufu kama Mo, amesema nusu fainali ya Ligi ya Mabigwa Afrika, haitakuwa na mvuto pasipo uwepo wa timu yake ya Simba.
Hii inakuja baada
ya wekundu wa Msimbazi, wakicheza soka safi katika mechi zote mbili za robo
fainali dhidi ya Kaizer Chiefs ya Afrika Kusini kutolewa kwa jumla ya mabao
4-3.
Katika mchezo wa
kwanza jijini Johannesburg Afrika Kusini, Simba ilipokea kipigo 'hevi' cha
mabao 4-0 na kwenye marudiano Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, wekundu
hao wa Msimbazi wakawapiga Kaizer mabao 3-0.

Post a Comment