MKOA WA CHATO WAZIDI KUPINGWA

HUKU michakato ikiwa imeanza kwa ajili ya kuiwezesha Chato kuwa Mkoa, wadau mbalimbali wamepinga jambo hilo na kudai watu waache kumshinikiza Rais Samia Suluhu Hassan kukubali kitu hicho, bali ashauri kwa nia ya kujenga.
Aliyewahi kuwa Waziri wa Ardhi Nyumba na
Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, alisema hakubaliana na suala hilo,
kwa vile anaamini eneo hilo jirani na nyumbani kwao, halina sifa za kuwa mkoa.
Pamoja na kuorodhesha sababu nyingi za kutokidhi
vigezo, lakini kubwa alilosema ni nchi kuacha kutoa maamuzi yenye lengo la
kuwaridhisha wakubwa, badala yake ifikirie mzigo mkubwa unaokwenda kwa walipa
kodi.
Mwingine aliyepinga
jambo la Chato kuwa mkoa, ni Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo
la Rulenge-Ngara Mhashamu Baba Askofu Severine Niwemugizi
ambaye alitumia Dominika ya leo kutoa
hisia, maoni zake kuhusu kuifanya Chato kuwa Mkoa.
Mwingine
aliyepinga wazo hilo ni Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula wa Kanisa la Moravian
la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.

Post a Comment