MIAMBA WATATU DAR WAINGIA NUSU FAINALI FA

SIMBA, Yanga na Azam, miamba ya soka Tanzania Bara ambao wanafukuzana kuwania ubingwa wa soka msimu huu, wote wamefanikiwa kuingia nusu fainali ya Michuano ya Azam Confederation Cup maarufu kama FA Cup msimu huu.
Hiyo inafuatia
ushindi wao katika mechi za robo fainali, Yanga ikiiondoa Mwandui FC katika
mchezo wao wa robo fainali, Azam wakiibenjua Rhino Rangers ya Tabora wakati
Mabingwa wa nchi, wakipata ushindi mbele ya Dodoma Jiji.
Katika nusu
fainali, mabingwa wa kihistoria Yanga, watapepetuana na Biashara Mara wakati
vigogo wawili wa Dar es Salaam, Simba na Azam, wakimtafuta wa kufika fainali.
Simba ndiyo
mabingwa watetezi wa michuano hiyo.

Post a Comment