LAZARO NYALANDU AREJEA SINGIDA

SIKU chache baada ya kurejea Chama Cha Mapinduzi (CCM) akitokea Chadema alikoelekea mwaka 2017 wakati
wa Mkutano mkuu maalumu, jana Lazaro Nyalandu alipokewa nyumbani kwao mkoani
Singida.
Katika shamra za kumpokea waziri huyo wa zamani wa Maliasili
na Utalii, aliambatana na viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani, akiwemo Dr
Robert Bujiku aliyekuwa mjumbe wa kamati kuu CHADEMA, Joyce Sokombi aliyekuwa
mbunge wa viti maalum CHADEMA 2015/2020 aliyekuwa mgombea ubunge kupitia NCCR
MAGEUZI jimbo la Musoma Mjini na katibu Mkuu wa wanawake NCCR Mageuzi (Taifa)
Bi Tabitha Mkube na Robert Mpemba aliyekuwa katibu wa CHADEMA mkoa wa Rukwa
walioamua kujiunga na CCM jana.
Wanachana hawa wapya wamepokelewa na Mwenyekiti wa UVCCM
Taifa, Kheri James katika ofisi za Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Singida.

Post a Comment