K VANT YAZUA MJADALA MITAANI


KVant Bottle Photography & ART on Behance

WAKATI kinywaji kikali aina ya K Vant kikiliteka soko la wanywaji wa pombe kali, hali imegeuka kuwa gumzo mitaani baada ya baadhi kudai 'ukipiga' hayo maji meupe, kumbukumbu zinapotea.

Kwa mujibu wa majadiliano hayo, wadau wanasema K Vant ni kinywaji supa sana na kwa kweli hivi sasa kipo juu kimahitaji sokoni, lakini tatizo lake ni hilo tu;

"Asikuambie mtu, mimi naipenda sana hii kitu, tatizo lake ni moja tu, kesho nitaamka nikiwa nimesahau mambo mengi ya jana yake, tofauti na nikinywa pombe zingine kali au bia," anasema mnywaji mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la Zomboko.

Kauli hiyo imeungwa mkono na watu wengine kadhaa ambao nao wamekiri kuwa licha ya uzuri wake, wanywaji wake wana tatizo la kupoteza kumbukumbu

No comments