JICHO LA TATU BAO LA BERNARD MORISSON

UKIONDOA mashabiki wachache wa watani wao wa jadi, Yanga, wengi wanakubaliana ndani ya mioyo yao kwamba Simba wako vizuri, ndani na nje ya uwanja. Why?
Ndani ya uwanja,
wana wachezaji wenye viwango, wanaogombania namba. Wana kocha mzuri anayejua
mbinu na ndiyo maana kutokuwepo kwa mchezaji yeyote, wa nafasi yoyote,
haijawahi kuwa excuse kwa wao kushindwa. Ikitokea Simba imefungwa, kwamba flani
hakuwepo, ni kauli ya wapinzani.
Nje ya Uwanja, they
are well treated. Sisemi kuhusu malipo, lakini wanafika eneo la tukio kwa
wakati, wanafikia hoteli ghali popote, iwe Tzee au nje na wana mashabiki
wanaowapenda.
Njoo kuhusu bao la
Morrison. Linatafsiri maana ya wachezaji wenye viwango. Kwanza unakubaliana na
mimi, Morisson siyo chaguo la kwanza kikosini Simba, inabidi asubiri, asome
mchezo then aingie ili alete tofauti.
Angalia lile bao
lake la tatu kwa Simba dhidi ya Namungo; only a quality player can score. Mita tano
tu kutoka katikati ya uwanja, anakunjuka na kupiga mpira wa vipimo, golikipa
mzuri anahangaika hadi basi. Hakuna aliyemlaumu kipa, bali walimpongeza
mpigaji.
Baada ya Azam Media
kutupia hizo bilioni 225, ni matumaini yangu timu zetu zisajili wachezaji wenye
viwango, ambao hata hapa Bongo wapo, ili ligi yetu isiwe ya upande mmoja. Just
imagine, timu zimecheza mechi 30, lakini inayoongoza imecheza mechi 26 tu, tena
ikiwa na idadi kubwa ya mabao ya kufunga na ikifungwa machache kuliko zote.
Weka ushabiki pembeni,
ligi yetu haina uwiano baina ya Simba na timu zingine.

Post a Comment