JEURI YA FEDHA KATIKA LEVO ZINGINE JAY Z NA BEYONCE
WANANDOA Jay-Z na Beyoncé ambao ni
moja ya couple zinazochukuliwa kama mfano kwa mastaa wa Marekani, wameandika
historia kwa mara nyingine tena kwa kuagiza kutengenezewa gari ghali zaidi
ulimwenguni.
Mtandao wa PageSix unaripoti kuwa
Jay Na Bey wamelipa US dola milioni 28, sawa na shilingi za kitanzania bilioni
64, kununua gari la kifahari aina ya Rolls Royce BoatTail Convertible
lililotengenezwa kutokana na matakwa yao.
Roll Royce ya Blue na imepambwa na
vitu vyote wanavyopenda Couple hii.
Jay Z na Beyonce hupenda kushirikiana kununua
vitu pamoja tofauti na wanandoa wengi maarufu duniani, tambua kwa sasa wanaishi
kwenye nyumba walionunua pamoja yenye thamani ya US Dola milioni 88 (Wanailipia
kwa muda wa miaka 30) kwenye mitaa wanayoishi mastaa na matajiri huko Bel-Air,
Los Angeles, California.
Jumba hilo lina vyumba 8 vya kulala,
mabafu 11, eneo la kuegesha magari 15, mabwawa ya kuogelea manne na uwanja wa
mpira wa kikapu.

Post a Comment