JAKAYA NI MZIMA WA AFYA - RIDHIWANI


Ridhiwan Jakaya Kikwete - Posts | Facebook

 KUMEKUWA na taarifa katika baadhi ya mitandao ya kijamii, ikisema kuwa Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Mrisho Kikwete ni mgonjwa. Habari hizo zinasambaa kwa kasi.

Hali hiyo imesababisha watu wa karibu na familia hiyo kupiga simu na kutuma ujumbe kwa wanafamilia wakitaka kujua ukweli.

Mtoto wa kiume wa Jakaya, ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete amekanusha taarifa za sintofahamu zilizosambaa kupitia mitandao ya kijamii zikimhusishia baba yake mzazi na rais mstaafu wa Tanzania, Dkt. Jakaya Kikwete.

Kupitia akaunti yake ya Twitter, Ridhiwan ameandika:
"Baada ya kupokea Simu na Jumbe mbalimbali nimeona nitumie nafasi hii kuweka kumbukizi sawa. Mzee wetu na Mzazi wetu Dr. Jakaya Mrisho Kikwete yupo salama wa afya nyingi sana. Hana tatizo lolote kiafya na anaendelea na majukumu yake. Taarifa za aina yeyote ni za Kipuuzi na za kupuuzwa"...

 

No comments