INAWEZEKANAJE DAWA ZIPULIZWE VYUMBA VYA WACHEZAJI?

KELELE za timu mbalimbali juu ya tabia ya timu moja kupuliza dawa katika vyumba vya wachezaji wapinzani zinazidi kuwa nyingi na ya hivi karibuni ni ya jana kutoka kwa viongozi wa klabu ya Dodoma Jiji wakiilalamikia Simba.
Katika
mchezo huo wa jana, wageni hao kutoka Dodoma walisalimu amri baada ya kupigwa
mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa katika dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es
Salaam.
Hizi
ni kelele za siku nyingi na mtuhumiwa namba moja mara nyingi amekuwa ni Simba.
Hebu tujiulize, jambo hili linawezekanaje na wahusika wote wabaki kimya?
Viongozi wa Uwanja
Huu
ni uwanja wa serikali na una uongozi wake kamili kwa maana ya meneja na
wafanyakazi waajiriwa. Kuna mtu mwenye jukumu la kuangalia sehemu ya kuchezea
(pitch), kuna mtu wa kusimamia usafi wa majukwaa, vyumba na mwisho kabisa
walinzi. Hivi hawa wote wapo wapi hadi jambo hili linafanyika kila siku?
Wizara ya Habari, Sanaa,
Utamaduni na Michezo
Hawa
ndiyo wasimamizi wa huu uwanja kwa niaba ya serikali. Ni jukumu lao kwa hiyo
kuhakikisha tuhuma kama hizi zinakomeshwa ama kwa kuanika ukweli au kukanusha.
Wizara
inao madaktari wa binadamu na inao wataalamu wa afya wenye uwezo wa kutambua
madawa ya aina mbalimbali. Wanaweza kujua chumba hiki, siku fulani kilipuliziwa
dawa aina hii, yenye madhara haya na yale. Mbona hawaifanyi hii kazi?
TFF mbona wananyamaza wakati
soka likichafuliwa?
Unashangaa
kwa nini Shirikisho la Soka nchini TFF linakaa kimya wakati mchezo wa soka
unachafuliwa. Kitendo cha timu kulalamikiwa kwa kupulizia dawa timu pinzani ili
icheze chini ya kiwango waweze kushinda, ni hujuma kwa TFF inayotaka soka la
haki na ushindani ndani ya uwanja.
TFF
ina wataalamu wa kujitegemea wenye uwezo wa kuondoa utata huu. Kama ni kweli
Simba wana tabia hiyo, ikithibitishwa, wachukuliwe hatua stahiki ili mradi
mchezo huu ubakie kuwa wa kuzingatia sheria 17.
Kama
lenyewe linashindwa, linaweza kuomba msaada kutoka Caf au hata Fifa ili mradi
malalamiko haya ambayo lengo lake ni kuipaka matope image ya soka la Tanzania
yaondolewe kabisa.
Simba wenyewe wanasemaje?
Ni
jambo la ajabu kidogo kuona wanaotuhumiwa mara nyingi, ambao ni Simba wamekaa
kimya. Inawezekana ni kweli wameamua kupuuza kwa sababu hawahusiki, lakini uongo
unaposemwa sana na wenye wajibu wa kukanusha wakakaa kimya, huonekana ni
ukweli.
Maana
isije ikawa kuna watu wanacheza na saikolojia ya timu pinzani. Watu wanaweza
kuja kupuliza manukato chumbani, lakini kwa hofu iliyojengwa, hujikuta
wakiamini ni dawa za kupunguza uwezo.
All
in All, wahusika lazima wasimame na kusema ukweli.

Post a Comment