CHADEMA YAKATAA KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU 2025

CHAMA Kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema hakitashiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 hadi pale Katiba Mpya itakapopatikana na kuwepo kwa Tume Huru ndani yake.
Msimamo
huo umetolewa na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe wakati
akizungumza katika kikao chake na viongozi wengine wa Kanda ya Kaskazini jijini
Arusha.
Jambo
hilo limezua maoni mengi tofauti kutoka kwa wadau na hivyo kusababisha hali
hiyo kuzua mjadala mkubwa katika mitandao ya kijamii hivi sasa.

Post a Comment