HAKUNA MISHAHARA MIPYA

 Samia Suluhu, the woman taking over Tanzania - The Standard

RAIS Samia Suluhu Hassan leo amehutubia katika kilele cha siku ya wafanyakazi duniani, lakini tofauti na matarajio ya wengi, amekataa kupandisha mishahara.

Amesema ni mapema mno kwake kuweza kupandisha mishahara wiki chache tu tangu achukue madaraka, lakini akatoa ahadi kuwa atafanya hivyo siku zijazo.

Hata hivyo, pamoja na mishahara kutokupanda, kodi ya mshahara inapunguzwa, Tozo ya asilimia 6 kwenye makato ya Bodi ya Mikopo imefutwa, watumishi wanapandishwa madaraja, na ukomo wa umri wa wategemezi kwenye Bima ya Afya umeongezwa kutoka miaka 18 hadi 21.

Wachumi wsengi hawakutegemea mishahara kupanda kwani kampuni na mashirika mengi, ya umma na binafsi yameyumba kutokana na athari za Covid-19.

 

No comments