GARI LA AKON LAIBWA KITUO CHA KUJAZIA MAFUTA


Best SUVs for 2021 - Roadshow

 TAARIFA iliyotolewa hivi punde na tovuti ya habari za burudani #TheShadeRoom imeripoti kuwa gari ya staa wa muziki kutokea nchini Senegal, Akon imeibiwa. 

Kwa mujibu wa #Fox5Atlanta gari hilo limeibiwa wakati ambapo nyota huyo akiwa katika kituo cha kujaza Mafuta huko Sydney Atlanta, ambapo mtuhumiwa alirukia ndani ya mchuma huo akaliwasha na kukimbia nalo.

Taarifa zinaeleza gari hilo aina ya SUV ndilo lililokuwa likimilikiwa na staa huyo na kuibiwa.

Hata hivyo, idara ya polisi ya Atlanta wapo katika uchunguzi ili kumbaini mtuhumiwa aliyehusika na kitendo hicho cha kihalifu.

No comments