ECOWAS NAYO YATISHIA KUIWEKEA MALI VIKWAZO VIPYA


Mahakama ya Mali yamtangaza Goita rais wa mpito | Matukio ya Kisiasa | DW |  29.05.2021

SIKU chache tu baada ya Marekani na Jumuia ya Ulaya kuonya juu ya kuiwekea vikwazo nchi ya Mali baada ya Jeshi kufanya mapinduzi, Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) nayo imeonya kuwa inaweza kurejesha vikwazo nchini humo kufuatia Kanali Assimi Goita kuchukua madaraka.

Kanali Goita ameitwa kwenye Mkutano wa Dharura wa Viongozi wa Afrika Magharibi Nchini Ghana ambapo mapinduzi ya pili ya Mali katika miezi 9 yatajadiliwa.

ECOWAS inahofia mabadiliko hayo yanaweza kuyumbisha utulivu na kudhoofisha mapigano ya Kikanda dhidi ya vikundi vinavyohusiana na Al-Qaeda na ISIS.

No comments