DRAKE AKODI UWANJA WA WATU 70,000, AWAPA MISOSI
AUBREY Graham, mmoja wa wasanii
wakubwa wa Hip Hop duniani ambaye ni maarufu kama Drake, amekamata headlines
mbalimbali za kiburudani, kufuatia hatua yake ya kuukodi uwanja wenye uwezo wa
kuingiza watu 70,000, kisha akawaingiza ndugu, jamaa na marafiki zake
kusherehekea tuzo aliyopata.
Drake kutoka Canada, alipata tuzo ya
msanii wa muongo Artist Of The Decade kutoka BBMAs na hivyo kuukodi Uwanja wa SoFi unaopatikana katika eneo la Inglewood,
jijini California.
Hata hivyo katika hafla hiyo pia #Drake alijumuika
pamoja na watu mbalimbali kama vile ndugu, jamaa na marafiki kwa ajili ya kujipatia
chakula cha usiku
Uwanja huo wa #SoFi ulipambwa kwa
kuchapishwa maneno kwenye mabango yaliyokuwa ndani ya uwanja huo kwa kusomeka
"Artist of the Decade"

Post a Comment