DIAMOND AENDA MSABAHI SHAKA LUMUMBA
NYOTA wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz leo alifika ofisi ndogo za Makao Makuu ya CCM, yaliyopo Lumumba jijini Dar es Salaam na kukutana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Mpya wa CCM Shaka Hamdu Shaka.
Katika ukurasa wake wa Instagram, mwekezaji huyo kijana
aliandika: "Nimetumia wakati huo kumng'ata sikio juu ya matarajio yetu kwa
Chama na Serikali katika Sekta ya Habari, Sanaa na Burudani, na amenihakikishia
changamoto zote zitafanyiwa kazi na tabasamu litazidi kuonekana.
"Mwisho, Kama Kijana nimefarijika kuona Mwenyekiti wangu
wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani
anaendelea kuamini Vijana katika nafasi mbalimbali za Uongozi ndani ya Chama na
Serikali, Katibu Mkuu wa CCM Kijana, Mwenezi Taifa wa CCM Kijana hili lina
maana kubwa katika hili na mpongeza sana na ninawaomba Vijana na Watanzania
wote wenzangu tumuunge Mkono, Mhe. Samia Suluhu Hassani ili mazuri aliyoyapanga
katika Uongozi wake yaweze kutimia."

Post a Comment