CRISTIANO RONALDO ATAMBAA NJIA YA JACKO WACKO
UNAMKUMBUKA Legendary wa muziki wa Pop duniani, Michael Jackson wa Marekani? Jamaa alikuwa anawazingua sana wamarekani weusi, hasa alipokuwa anafanya juhudi kubwa kuukana weusi wake, akitaka kujifananisha na wazungu.
Hata hivyo, uwezo wake na ubunifu
wake kazini, ulimfanya apate heshima kutoka jamii za watu wote wa taifa hilo
kubwa zaidi duniani. Na kuna jambo moja alilolifanya, likamfanya awe wa
kipekee.
Jamaa hakuwahi kuoa ingawa alifariki
akiwaacha wanae watatu. Hawa wote aliwapata kwa makubaliano na mama zao,
akipandikiza mbegu. Hii maana yake ni kuwa vijana wale wa Jacko Wacko, hawamjui
mama yao.
Hivi ndivyo ilivyo kwa mwanasoka nyota
duniani, Cristiano Ronaldo.
Mtoto wa kwanza wa Ronaldo, Cristiano jr, ni mtoto
aliyetokana na makubaliano ya kimkataba kati ya nyota huyo na mwanamke mmoja
nchini Marekani, ambako kazi yake ni kuzaa tu, baada ya hapo analipwa chake
maisha yanaendelea.
Mkataba ulisema baada ya kuzaa, atalipwa pesa na hivyo kupoteza haki zote za mtoto na haruhusiwi kujitangaza, vinginevyo atalazimika kulipa malipo makubwa.
Kitendo hiki kinaitwa Surrogacy, mama anayezaa mtoto anaitwa
Surrogate Mother, ni makubalino ya kisheria, ukasainiwa kati ya Ronaldo na mwanamke
mbele ya Wanasheria wa pande zote mbili.
Hii pia hakuishia kwa Cristiano Jr tu bali hata watoto wake mapacha
Mateo na Eva nao walizaliwa kwa mkataba kati ya Mama wa watoto na Ronaldo.

Post a Comment