CCM PIA WAIBUKA WASHINDI JIMBO LA BUHIGWE

 


IMG-20210517-WA0004.jpg

FELIX Kavejuru ambaye aligombea Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika jimbo la Buhigwe, ametangazwa kuwa mshindi wake baada ya kuwabwaga wapinzani wake 12 wengine.

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Buhigwe, Marycelina Mbehoma alimtangaza Felix Kavejuru katika uchaguzi uliofanyika Mei 16, 2021, kwamba alipata kura 25,274 kati ya kura 30320 halali zilizopigwa. Hivyo Ndugu Felix Kavejuru ndiye Mbunge mteule jimbo la Buhigwe kwa tiketi ya CCM.

Uchaguzi huo ulifanyika ili kuziba nafasi iliyoachwa wazi baada ya alikyekuwa mbunge wake, Philip Isdor Mpango kuteuliwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kufuatia kifo cha Rais John Joseph Magufuli.

 

 

No comments