BOSI WA YANGA KUMJENGEA NYUMBA MWAKINYO

 

Mfanyabiashara Davis Mosha akamatwa na Askari wa Uhamiaji - YouTube

MFANYABIASHARA maarufu nchini ambaye pia aliwahi kuwa kiongozi wa Klabu ya Yanga, ambao ni mabingwa wa kihistoria katika Ligi Kuu Bara, Davis Mosha ameahidi kum-support Bondia Mtanzania Hassan Mwakinyo  kwenye mambo mbalimbali ikiwemo kwenye ujenzi wa nyumba yake.

“Ni kijana anapenda fani yake nimeona nim-support kwenye mambo mengi kwa mfano akija Dar es salaam huwa mimi ndio nam-take care kila kitu na nina zawadi niliahidi nitampa sababu ametufurahisha Watanzania” 

“Kuna mambo mengi nimemuahidi kum-support, nimemwambia sasa hivi atafute kiwanja ili tuweze kum-support aweze kujenga nyumba yake na mimi ni miongoni mwa Watu wanaotaka kum-support ajenge nyumba yake”

Juzi, Mwakinyo alimtwanga bondia kutoka Angola na kufanikiwa kutwaa mkanda wa Afrika.

 

No comments