ASKARI WATATU WASIMAMISHWA UHAMIAJI

IDARA ya uhamiaji imewasimamisha
kazi askari wake watatu kwa tuhuma za kutumia nguvu kinyume cha sheria na
maadili ya kazi zao dhidi ya mtuhumiwa wa utapeli Alex Raphael Kyai kama
ilivyoonekana katika video fupi iliyosambaa.
Mtuhumiwa huyo anadaiwa kulaghai na kupokea fedha kutoka kwa
wateja mbalimbali ili waweze kupata pasipoti kwa haraka pia amekuwa
akijitambulisha kama Mtumishi wa Taasisi nyeti ikiwemo TAKUKURU.
"Hatua ambazo Idara imechukua dhidi ya askari,
tumewasimamisha kazi kupisha uchunguzi wa tukio lenyewe lakini pia Mtuhumiwa
tumemfikisha kwenye mamlaka husika ili aweze kuendelea na utaratibu mwingine
kisheria," amesema Dr. Anna Peter
Makakala, Kamishina Jenerali wa Uhamiaji.

Post a Comment