AMOS MAKALA AIKOROGA DAR ES SALAAM
SIKU chache tu baada ya kutamka kuwa ana mpango wa kuwarudisha makwao wananchi wote wanaofanya kazi ya kuomba mitaani jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Mkoa huo, Amos Makalla, sasa amewageukia wafanyabiashara ndogondogo maarufu kama machinga.
Makala amewaagiza Wakurugenzi Watendaji
wa halmashauri zote za mkoa huo kuwapanga upya wafanyabiashara hao.
RC Makalla ametoa agizo hilo alipokutana na watendaji wa Mkoa
wa Dar es Salaam ambapo amewaeleza vipaumbele vyake huku akisisitiza kuwa
hafurahishwi na mfumo wa ufanyaji biashara kiholela unaotumiwa na
wafanyabiashara hao hivi sasa.

Post a Comment