KIDUKU AKATAZA SKIN JEANS KOREA KASKAZINI
WAKATI vijana kote duniani wakifurahia zama zao kwa kuvaa suruali za kubana maarufu kama Skin Jeans na wakati huo huo wakizilegeza kamalioni, hali ni tofauti nchini Korea Kaskazini.
Rais kijana wa taifa hilo, Kim
jong-un ambaye ni maarufu hapa nyumbani kama Kiduku kutokana na aina yake ya
unyoaji nywele, amepiga marufuku kali jinzi na suruali zinazobana, akihofia raia
wa nchi hiyo kuiga utamaduni wa kimagharibi.
Kwa Korea Kaskazini kufuata falsafa ya Kikomunisti, imejitengenezea
maadui wengi duniani, hasa Ulaya na Marekani ambao wanapinga mfumo wao wa
utawala.
Kwa mujibu wa shirika la habari la "Yohap News"
kutokea Korea Kusini limelinukuu jarida la Korea Kaskazini katika moja ya
machapisho yake limesisitiza kuzuia mila za kimagharibi kuingia nchini humo au
wananchi wawe tayari kuona mila na tamaduni zao kupotea hivi hivi.
Kwa maana hiyo, chunga sana ikitokea unaelekea mitaa hiyo ya
dunia.

Post a Comment