TETESI: DIAMOND AMENUNUA PRIVATE JET?

Kuna tetesi zinasambaa mitandaoni kuwa msanii mkubwa Tanzania, Diamond Platnum amenunua ndege binafsi.
Vipande vya video
vinavyotoka kwa mmoja wa mameneja wake, Sallam zinaonyesha picha za mwekezaji
huyo kijana akiingia katika 'show room' ya ndege ndogo, ishara kwamba amekwenda
kwa ajili ya malipo.
Aidha, katika
akaunti yake kwenye mtandao wa Instagram, msanii huyo ameweka maneno ya
kushukuru, akisema Alhamdulilah, jambo linalotafsiriwa kuwa huenda ni kwa
kutimiza ndoto zake za muda mrefu.
Miaka kadhaa iliyopita,
mwimbaji huyo kutoka Tandale aliwahi kudokeza kuwa ana lango la kununua ndege
binafsi ili kurahisisha shughuli zake za kisanii na kibiashara.

Post a Comment