SIMBA YAENDA KUKAMILISHA RATIBA CAIRO

KWA mara ya kwanza
katika historia ya soka la Tanzania, klabu yake inaingia katika hatua ya robo
fainali ya Klabu Bingwa Afrika ikiwa inaongoza kundi lake.
Simba ndiyo imekuwa
klabu ya kwanza ya Tanzania kufanya hivyo, tena ikiwa na mechi moja mkononi.
Wakiwa safarini kuelekea Cairo nchini Misri, mabingwa hao mara tatu mfululizo wa
Ligi Kuu Tanzania Bara, wanaongoza kundi A wakiwa na pointi 13 baada ya mechi
tano.
Wanakwenda Cairo
nchini Misri kupambana na mabingwa watetezi wa klabu bingwa Afrika, Al Ahyl,
katika mechi ambayo matokeo yake yoyote hayawezi kuathiri uongozi wa Simba,
kwani hata wakifungwa, watakuwa mbele kwa alama mbili.
Mechi hiyo ya
kukamilisha ratiba itafanyika Jumamosi hii na wengi wanataraji wekundu hao wa
Msimbazi kuweza kuweka rekodi nyingine baada ya kuwa klabu ya kwanza Tanzania
kuongoza hatua za makundi ikiwa na mechi moja mkononi, kucheza mechi tano za
mashindano hayo ikiwa haijapoteza hata mchezo mmoja, kufungwa mabao machache
zaidi kuliko timu zote na kucheza kwa kiwango kikubwa (ball possession) katika
mechi zote.

Post a Comment