CHAMA MCHEZAJI BORA WA WIKI CAFCL

 

KIUNGO mtengeneza mipango wa Simba, Clatous Chota Chama 'Triple C' au maarufu kama Mwamba wa Lusaka, ameteuliwa kuwa mchezaji bora wa raundi ya tano ya michuano ya Klabu Bingwa Barani Afrika.

Katika mchezo wa raundi ya tano uliochezwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam April 3 mwaka huu, kati ya Simba na AS Vita, Chama alifunga mabao mawili na kutoa assist moja na hivyo kuhusika katika mabao matatu.

Hii ni mara ya pili kwa klabu ya Simba kutoa mchezaji bora wa wiki katika michuano hiyo. Mara ya kwanza ilikuwa ni katika mchezo wa raundi ya pili katika ya Simba na Al Ahly jijini Dar es Salaam, ambapo mchezaji Luis Minniqsonne alifunga bao pekee la ushindi kwa Simba na bao lake likiwa ni bora wiki hiyo.

No comments