SENEGAL, TISHIO LA TANZANIA TIMU NNE MSIMU UJAO

SIYO habari rafiki
sana kwa familia ya soka nchini Tanzania, kwani hadi jana, bado hakuna uhakika
wa asilimia mia moja kuingiza timu nne katika kampeni za michuano ya kimataifa
ya Afrika.
Hii ni baada ya
jana, Al Ahli Benghazi ya Libya ikiwa ugenini kwenye mchezo wa mwisho wa kombe
la shirikisho (Caf Confederation Cup) kufungwa 1-0 na Es Setif ya Algeria na kushindwa
kufuzu robo fainali. Baada ya Benghazi
kushindwa kufuzu, nchi ya Libya imebaki na pointi 13.5 ambazo haziwezi
kuongezeka.
Tanzania baada ya
timu ya Simba kufuzu robo fainali ya Caf Champions League na Namungo kumaliza
nafasi ya nne kwenye makundi ya Caf Confederation Cup, sasa tuna pointi 27.5
ambazo zinaweza kuongezeka ikiwa Simba itafanikiwa kufuzu nusu fainali ya Klabu
bingwa Afrika.
Baada ya Libya
kushindwa, mshindani wetu kwa sasa ni Senegal ambayo haikuwa na pointi zaidi ya
timu zao 2 kufanya vizuri msimu huu ambazo ni timu ya Teungueth FC iliyoshiriki
klabu bingwa Afrika na kuishia nafasi ya nne kwenye makundi huku ASC Jaraaf
imefanikiwa kufuzu robo fainali ya kombe la shirikisho kama nchi Senegal wana
Pointi 15 sasa.
-Nchi ya Senegal
pointi zake zinaweza kuongezeka kwa sababu ya Klabu ya ASC Jaraaf kufuzu robo
fainali ya kombe la shirikisho (Caf Confederation Cup) ila mpaka atuzidi sisi
Tanzania mpaka timu yao ya ASC Jaraaf iwe bingwa wa Kombe la Shirikisho
(atakuwa amefikisha pointi 30) huku aiombee timu ya Simba itolewe robo fainali
ili sisi (Tanzania) tubaki na Pointi 27.5

Post a Comment