LEICESTER WAHOFIA KUTUPWA TENA NJE CL

 Brendan Rodgers insists Leicester's flat performance against Brighton has  nothing to do with playing behind closed doors

KLABU ya soka ya Leicester ambayo hadi sasa inashika nafasi ya tatu katika Ligi Kuu ya England, inahofia huenda ikatupwa nje ya michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya kwa mara pili mfululizo, HATA KAMA itamaliza ikiwa ndani ya Top Four.

Hata hivyo, hiyo itatokea tu iwapo Chelsea na Arsenal zitashinda makombe ya Ulaya, ambako timu hizo mbili zimefikia hatua ya fainali.

Chelsea inashiriki Ligi ya Mabingwa wakati washika mitutu wa London, wapo Europa League.

Kikosi hicho cha kocha Brendan Rodgers kipo katika nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa na pointi 62, nne nyuma ya Chelsea. Ili kucheza michuano ya Ulaya mwakani, italazimika kupigana kuhakikisha inamaliza ligi ikiwa nafasi hiyo hiyo.

Lakini wakishika nafasi ya nne, na majirani hao wa London wakashinda mataji, watajikuta nje ya michuano ya Ulaya kwa vile Shirikisho la soka barani Ulaya, hutoa nafasi hadi tano tu kwa timu za nchi moja kushiriki michuano yake.

Msimu uliopita, Leicester nusura icheze Ligi hiyo ya Mabingwa baada ya kufanya vyema kabla ya kuporomoka kiwango kufuatia lockdown ya Covid 19 na kujikuta wakipokea kipigo toka kwa Man United katika mechi yao ya mwisho iliyowafanya wacheze Europa League.

No comments