NYALANDU, METHEW WAREJEA CCM
ALIYEWAHI kuwa
Waziri wa Maliasili na Utalii katika serikali ya Awamu ya nne, Lazaro Nyalandu ambaye
alikihama chama hicho Septemba mwaka 2017 na kujiunga na chama kikuu cha
Upinzani nchini, Chadema, amerejea katika chama tawala.
Nyalandu ambaye
alikuwa ni Mwenyekiti wa Kanda ya Kati
wa Chadema na Mjumbe wa Kamati Kuu,
amejiunga na chama hicho leo, wakati wa mkutano mkuu maalum uliokuwa na lengo
la kumkabidhi Rais Samia Suluhu Hassan Uenyekiti wa chama hicho kikongwe.
Wakati wa hotuba
yake mbele ya mkutano huo, Nyalandu, pamoja na mambo mengine, aliwaomba radhi
wanachama wa CCM kwa kitendo chake hicho cha kuhama chama.
Wakati huo huo,
aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kusini, Seleman Methew naye amejiunga
na chama hicho tawala, akidai ndicho kilichomkuza kisiasa.

Post a Comment