SEKRETARIETI MPYA CCM KUTANGAZWA LEO

MAKAMU Mwenyekiti
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Philip Mangula amesema baada ya kumchagua
Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Samia Suluhu Hassan, kazi itaendelea ili
kuiteua na kuitangaza Sekretarieti mpya.
Moja ya nafasi
inayosubiriwa kwa hamu kubwa ni ile ya Katibu Mkuu wa chama hicho ambayo
imekuwa wazi tangu Bashiru Ally Kakurwa alipoteuliwa na baadaye kuondolewa kuwa
Katibu Mkuu Kiongozi.
"Zege
halilali," alisema Mwenyekiti Mpya Mama Samia wakati akiufunga rasmi
mkutano mkuu maalum, huku akiwataka wajumbe wa Halmashauri Kuu kuendelea
kusubiri ili kuimaliza kazi hiyo leo hii hii.

Post a Comment