PRESHA WAKUU WA MIKOA, WILAYA, MADED
BAADA ya Rais Samia
Suluhu Hassan kufanya marekebisho kadhaa katika nafasi za Mawaziri, Manaibu
Mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi, Makatibu Wakuu wa Wizara, Manaibu Makatibu Wakuu na Taasisi za Serikali, sasa yu
mbioni kufanya hivyo kwa Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri.
Presha kwa viongozi
hao wa kisiasa imepanda, kwani hakuna mwenye uhakika wa kubakia kwenye nafasi
yake, achilia mbali kubadilishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine.
Wakatgi wa uongozi
wake, Rais wa Awamu ya Tano, John Joseph Pombe Magufuli, aliwapa nafasi hizo
baadhi ya watu walioonekana kama wenye kujipendekeza, kumsifu kupita kiasi na
ambao sifa yao kubwa ilikuwa ni kuwanyanyasa wapinzani wa CCM.
Baadhi ya wakuu wa
mikoa, wilaya na wakurugenzi wamekuwa wakilaumiwa na wananchi wa maeneo yao,
wakionekana kutofanya kazi zao sawasawa, hivyo kutamani mabadiliko kutoka kwa
Mama Samia maarufu kama Sasha.

Post a Comment