MSIKIE RYAN GIGGS AKIMZUNGUMZIA KAKA!!!




Ricardo Kaka announces his retirement - EgyptToday


KAMA kuna mchezaji ambaye  ninahisi kumpenda ndani ya moyo wangu kwa uwezo wake uwanjani, uungwana wake, hadhi yake na ubinadamu, bila shaka yoyote atakuwa ni Ricardo Kaka.

Tulikutana katika nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa pale Old Trafford na Kaka alikuwa hakabiki, alikuwa na kiwango ambacho kilikuwa cha juu mno katika yale mashindano ambacho kilileta tofauti. Ilikuwa ni mara yetu ya kwanza kukutana uwanjani.

Kuna wakati katikati ya uwanja nilimchezea faulo, akanisogelea na kunikaba shingoni na yeye alipewa kadi kwa kitendo hicho. Nilijua wakati huo kuwa alikuwa ni mtu wa dini na ameokoka, lakini nikajiuliza, mtu wa imani kiasi hicho anawezaje kunikaba hivi?

Mchezo ulipoisha tukiingia katika vyumba vyetu vya kubadilishia nguo, alikuwa akinisubiri akiwa na Gennaro Gattuso ambaye alikuwa akiongea Kiingereza vizuri kwa sababu aliwahi kuichezea Rangers.

Gattuso aliniambia kuwa Ricardo alitaka kuniomba radhi kwa kitendo chake kisicho cha kiungwana alichonifanyia. Nikasema haina taabu, sisi wote ni binadamu.

Ricardo alinikumbatia na akanipatia msalaba. Nilishtuka sana kwa uungwana wake na nikamwambia "Ricardo, usijali, wachezaji wakiwa uwanjani wakati mwingine hufanya mambo ya ajabu sana, lakini katika Ligi ya Mabingwa na hasa katika mchezo wa Nusu Fainali, hivi ni vitu vya kawaida.

Gattuso alifanya vizuri sana katika kutafsiri na Kaka akapiga magoti mbele yangu na akanishukuru tena. Wachezaji wote ndani ya chumba cha kubalishia nguo walishangilia na tukabadilishana jezi. Zawadi yake bado ninayo na inanikumbusha moja kati ya matukio muhimu zaidi katika maisha yangu ya soka.

No comments