MTUKUTU MARIO BALOTELLI ANAPOPATA UFAHAMU!!
"Ninawaomba wachezaji wote wenye asili kutoka Afrika tuweke pesa sehemu moja tuipe thamani Afrika.
Tuna uwezo wa kifedha, nina
imani hiyo kabisa kwa pamoja twaweza kujenga viwanja vitano vya kifahari kwa kila
nchi halafu tunaunda michuano yetu na sisi ili tuwe na amani na sisi kuhusu
rangi yetu, tuwapishe wazungu na ardhi yao ambayo kila kukicha matatizo
yanakuwa zaidi, kisa tu tuko Waafrika na ngozi yetu nyeusi hawaipendi.
Afrika Kuna vipaji vingi na
vinakosa sapoti kwa hiyo sisi wachezaji ambao tayari tuna kipato tunaweza
kukuza zaidi vipaji vya Afrika huku tukiweka michuano na sisi mfano Champions
league yenye nguvu na yenye thamani halafu tukakubaliana kuwa hakuna mchezaji
kutoka Afrika atacheza tena Ulaya, yote yanawezekana ingawa nitapata watu ambao
watapingana na mimi."

Post a Comment