MADAM SAMIA SULUHU HASSAN MWENYEKITI CCM

 Samia Suluhu, the woman taking over Tanzania - The Standard

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan maarufu kama Sasha, leo atapewa nafasi ya Uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, mbele ya Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho kikongwe.

Hii inafuatia kifo cha Mwenyekiti aliyetangulia, John Pombe Magufuli, ambaye alifariki dunia Machi 17 mwaka huu kwa ugonjwa wa moyo katika Hospitali ya Mzena, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Maandalizi yote ya mkutano huo yamekamilika na wajumbe wote wameshawasili jijini Dodoma, tayari kwa mkutano huo utakaofanyika katika ukumbi wa chama hicho.

Wakati Mama Samia akikabidhiwa nafasi hiyo ya juu kabisa katika chama hicho, Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Dk. Mohamed Shein, naye anatarajiwa kumkabidhi wadhifa huo Rais wa sasa wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi.

No comments