KAGERE, DUBE WACHUANA KILELENI

Prince Dube, mshambuliaji nyota wa
Azam, amefikisha mabao 11 katika Ligi Kuu Tanzania Bara, sasa akiwa anapambana
na washambuliaji wa Simba Meddie Kagere mwenye idadi kama hiyo ya mabao na John
Bocco ambaye ameingia kambani mara kumi.
Washambuliaji wengi wameshindwa kupambana na Kagere tangu
ameingia nchini kwa sababu misimu yote aliyocheza VPL amekuwa mfungaji bora.
Mazingira ya Dube na Kagere msimu huu yanafanana kwa kiasi
fulani, wote wamekosa baadhi ya mechi za ligi, Dube alipata majeraha na akakaa
kwa muda nje ya uwanja lakini Kagere anaathiriwa na makocha wa timu yake
kufanya rotation kwenye eneo la ufungaji.
Kagere amekuwa hana uhakika wa kucheza mfululizo kama
ilivyokuwa misimu miwili iliyopita lakini hawa watu [Dube na Kagere] wanatuonesha
kuwa, kazi ya kufunga wanaweza kuifanya kwa ufasaha ndio maana pamoja na
kucheza mechi chache bado wanashindana kwenye orodha ya wafungaji.

Post a Comment