MSIKIE JOSE MOURINHO KWA MARIO BALOTELI

NINGEWEZA kuandika kitabu cha
kurasa 200 katika miaka yangu miwili nikiwa na Inter
Milan na Mario, lakini kitabu hicho kisingekuwa cha maana, kingekuwa ni
vichekesho.
Nakumbuka kuna wakati mmoja
tulienda kucheza na Kazan katika Ligi ya Mabingwa. Katika mechi ile
washambuliaji wangu wote walikuwa majeruhi, hakukuwa na Diego Milito wala Samuel
Eto’o, hakika nilikuwa katika kikaango na mtu pekee niliyekuwa naye alikuwa ni
Mario.
Mario alipewa kadi ya njano
katika dakika ya 42, kwa hiyo wakati wa mapumziko nilitumia dakika 14 kati ya
15 kuzungumza naye.
“Nilimwambia, Mario, siwezi
kukutoa, sina mshambuliaji katika benchi, kwa hiyo usimguse mtu, wewe cheza
mpira tu, ukinyang'anywa mpira tulia, mtu akikupa presha, wewe mpuuze, refa
akikosea, wewe uchune,
Dakika moja tu baada ya mpira
kuanza, kadi nyekundu!

Post a Comment