Bilionea ahukumiwa kifo kwa ulaghai wa dola bilioni 44 nchini Vietnam

 

Ilikuwa ni kesi ya kuvutia zaidi kuwahi kutokea nchini Vietnam, ikihusisha mojawapo ya ulaghai mkubwa zaidi wa kibenki ambao Vietnam haijawahi kuona.

Ndani ya ukumbi mzuri wa mahakama ya tangu enzi ya ukoloni katika Jiji la Ho Chi Minh, mfanyabiashara wa Kivietinamu mwenye umri wa miaka 67 alihukumiwa kifo siku ya Alhamisi kwa kuibia pesa katika moja ya benki kubwa zaidi nchini humo kwa kipindi cha miaka 11.

Truong My Lan alipatikana na hatia ya kuchukua dola za Kimarekani bilioni 44 – kama mkopo kutoka benki ya Saigon Commercial. Hukumu hiyo inamtaka arejeshe dola bilioni 27, pesa ambayo waendesha mashitaka wanasema ni ngumu kurejeshwa.

Watu 2,700 waliitwa kutoa ushahidi, huku waendesha mashtaka 10 na mawakili wapatao 200 wakihusika. My Lan ni miongoni mwa wanawake wachache waliohukumiwa kifo katika nchi hiyo.

Ushahidi ulikuwa katika masanduku 104 yenye uzito wa tani sita. Washtakiwa wengine 85 walishtakiwa na Truong My Lan, ambaye alikana kufanya makosa.

No comments