Watalii 482 waliotembelea Lindi waahidi kuitangaza Tanzania

 

KIASI cha watalii 482 kutoka nchi mbalimbali barani Ulaya waliotembelea Kisiwa cha Mafia, wilayani Mafia Mkoani Pwani mwishoni mwa wiki, wameahidi kuitangaza Tanzania huko waendako.

Wakiwa wamepokewa na Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Aziza Mwangosongo, watalii hao baada ya kufika kisiwani hapo, licha ya kufurahia manzari nzuri ya kisiwa hicho, lakini pia walijivinjari kwa muziki wa kopi uliopigwa na wao wenyewe, wakinakili muziki wa hayati Bob Marley.

Aisha, wakiwa ufukweni, watalii hao waliogelea na kupunga upepo, huku wakiangalia pia samaki wa aina mbalimbali wanaopatikana katika Bahari ya Hindi iliyopo Kisiwani hapo, ambapo waliwasili kwa meli kubwa ya kitalii duniani inayofahamika kama The World.

No comments