Vita vya Israel na Gaza: EU yasema njaa inatumika kama silaha

 


Njaa inatumika kama silaha ya vita huko Gaza, mkuu wa sera za kigeni wa EU amedai.

Joseph Borrell alielezea ukosefu wa msaada unaoingia katika eneo hilo kama janga lililosababishwa na "mwanadamu".

Meli ya Kihispania iliyobeba chakula kinachohitajika sana imeondoka Cyprus kuelekea Gaza, lakini Umoja wa Mataifa unasema hii haiwezi kuchukua nafasi ya utoaji wa misaada kwa njia ya ardhi.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu naye ameapa kuendelea na mashambulizi kusini mwa Gaza.

Njia ya haraka na mwafaka zaidi ya kupata msaada katika eneo hilo ni kwa njia ya barabara, lakini mashirika ya misaada yanasema vizuizi vya Israel vinamaanisha sehemu ya kile kinachohitajika ni kuingia.

Badala yake badala yake angalizo limeelekezwa kwa njia mbadala zikiwemo uwasilishaji wa misaada kwa kutumia njia za baharini na angani.

Israel inasema haina chakulaumiwa kwa uhaba wa chakula Gaza kwani inaruhusu msaada kupitia njia mbili za kusini.

Lakini akihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa mjini New York siku ya Jumanne, Bw Borrell alisema mzozo wa kibinadamu katika eneo hilo ulitokana na ukosefu wa njia za nchi kavu.

"Sasa tunakabiliwa na idadi ya watu wanaopigania maisha yao," alisema.

"Msaada wa kibinadamu unahitaji kuingia Gaza, na Umoja wa Ulaya unafanya kadri tuwezavyo ili kuwezesha hilo.

"[Mgogoro wa kibinadamu umesababishwa] na mwanadamu na tunapotafuta njia mbadala za kutoa usaidizi kwa njia ya baharini na anga, inabidi tujikumbushe kwamba tunapaswa kufanya hivyo kwa sababu njia ya asili ya kutoa msaada kupitia barabara ni kuwa… imefungwa kwa njia isiyo halali.

"Njaa inatumika kama silaha ya vita na tuliposhutumu tukio hili nchini Ukraine, tunapaswa kutumia maneno yale yale kwa kile kinachotokea Gaza."

BBC

No comments